Maisha Mapya

Basi kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili, ninyi pia jiimarisheni kwa nia hiyo hiyo kwa maana mtu aliyekwisha kuteseka katika mwili hana uhusiano tena na dhambi. Matokeo yake ni kwamba, kwa muda wa maisha yake yaliyobakia hapa duniani, haishi tena kwa kufuata tamaa mbaya za mwili bali anaishi kwa kufuata mapenzi ya Mungu. Maana mmekwisha kutumia muda wa kutosha katika maisha yenu yaliyopita mkifanya yale ambayo watu wasiomjua Mungu hupenda kutenda: uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulevi na ibada ovu za sanamu. Wanaona ajabu kwamba sasa hamshi riki tena pamoja nao katika ufisadi wao wa kinyama, nao huwatu kana. Lakini itawabidi kujieleza mbele zake yeye aliye tayari kuwahukumu walio hai na waliokufa. Kwa maana hii ndio sababu Injili ilihubiriwa hata kwa hao waliokufa: wahukumiwe kama wana damu wengine kuhusu maisha yao katika mwili, bali wapate kuishi katika roho kama Mungu aishivyo.

Kuja Kwa Kristo Kumekaribia

Mwisho wa mambo yote umekaribia. Kwa hiyo muwe na akili timamu na wenye kiasi ili mweze kuomba. Zaidi ya yote, pen daneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi sana. Karibishaneni pasipo manung’uniko. 10 Kila mmoja na atumie kipawa alichopewa kuwahudumia wengine, kama mawakili waaminifu wa neema mbalimbali za Mungu. 11 Mtu akisema kitu, basi na awe kama anayesema maneno halisi ya Mungu. Mtu anayetoa huduma na ahudumu kwa nguvu apewayo na Mungu; ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo. Yeye ni mwenye utukufu na uweza, milele na milele. Amina.

Kuteseka Kwa Mkristo

12 Wapendwa, msishangae kwa ajili ya mateso makali yanayowa pata kana kwamba ni kitu kigeni kinawatokea. 13 Bali furahini kwamba mnashiriki katika mateso ya Kristo, ili mpate kufurahi na kushangilia wakati utukufu wake utakapofunuliwa. 14 Kama mkilau miwa kwa ajili ya jina la Kristo, mmebarikiwa, kwa sababu Roho wa Utukufu, yaani Roho wa Mungu, anakaa juu yenu. 15 Lakini asiwepo mtu ye yote kati yenu ambaye atateswa kwa kuwa ni mwuaji, au mwizi, au mhalifu au anayejiingiza katika mambo ya watu wengine. 16 Lakini kama mtu akiteseka kwa kuwa ni mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu kwa jina hilo. 17 Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya watu wa Mungu; na kama itaanza na sisi, mwisho wa hao ambao hawatii Injili ya Mungu utakuwaje? 18 Na, “Kama ni vigumu kwa mtu wa haki kuokolewa, itakuwaje kwa mtu asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?” 19 Basi wale wanaoteswa kufuatana na mapenzi ya Mungu, wajikabidhi kwa Muumba wao aliye mwaminifu.

Living for God

Therefore, since Christ suffered in his body,(A) arm yourselves also with the same attitude, because whoever suffers in the body is done with sin.(B) As a result, they do not live the rest of their earthly lives for evil human desires,(C) but rather for the will of God. For you have spent enough time in the past(D) doing what pagans choose to do—living in debauchery, lust, drunkenness, orgies, carousing and detestable idolatry.(E) They are surprised that you do not join them in their reckless, wild living, and they heap abuse on you.(F) But they will have to give account to him who is ready to judge the living and the dead.(G) For this is the reason the gospel was preached even to those who are now dead,(H) so that they might be judged according to human standards in regard to the body, but live according to God in regard to the spirit.

The end of all things is near.(I) Therefore be alert and of sober mind(J) so that you may pray. Above all, love each other deeply,(K) because love covers over a multitude of sins.(L) Offer hospitality(M) to one another without grumbling.(N) 10 Each of you should use whatever gift you have received to serve others,(O) as faithful(P) stewards of God’s grace in its various forms. 11 If anyone speaks, they should do so as one who speaks the very words of God.(Q) If anyone serves, they should do so with the strength God provides,(R) so that in all things God may be praised(S) through Jesus Christ. To him be the glory and the power for ever and ever. Amen.(T)

Suffering for Being a Christian

12 Dear friends, do not be surprised at the fiery ordeal that has come on you(U) to test you, as though something strange were happening to you. 13 But rejoice(V) inasmuch as you participate in the sufferings of Christ,(W) so that you may be overjoyed when his glory is revealed.(X) 14 If you are insulted because of the name of Christ,(Y) you are blessed,(Z) for the Spirit of glory and of God rests on you. 15 If you suffer, it should not be as a murderer or thief or any other kind of criminal, or even as a meddler. 16 However, if you suffer as a Christian, do not be ashamed, but praise God that you bear that name.(AA) 17 For it is time for judgment to begin with God’s household;(AB) and if it begins with us, what will the outcome be for those who do not obey the gospel of God?(AC) 18 And,

“If it is hard for the righteous to be saved,
    what will become of the ungodly and the sinner?”[a](AD)

19 So then, those who suffer according to God’s will(AE) should commit themselves to their faithful Creator and continue to do good.

Footnotes

  1. 1 Peter 4:18 Prov. 11:31 (see Septuagint)