Basi, acheni kabisa uovu wote, hila yote, unafiki, wivu na masingizio yote. Kama watoto wachanga, mtamani maziwa safi ya kiroho, ili kwa hayo mpate kukua katika wokovu wenu, kwa maana mmekwisha kuonja fadhili za Bwana.

Jiwe Hai Na Taifa Takatifu

Basi, njooni kwake yeye aliye Jiwe lililo hai, ambalo lili kataliwa na watu bali kwa Mungu ni teule na la thamani kubwa. Ninyi pia, kama mawe hai mjengwe kuwa nyumba ya kiroho, mpate kuwa makuhani watakatifu, mkitoa sadaka za kiroho zinazokubaliwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo. Kwa maana imeandikwa katika Maandiko: “Tazama, ninaweka jiwe kuu la msingi huko Sayuni; jiwe la pembeni teule na la thamani kubwa, na kila amwaminiye hataaibika.” Kwenu ninyi mnaoamini, yeye ni wa thamani kubwa. Lakini kwao wasioamini, “Lile jiwe walilokataa waashi limekuwa jiwe kuu la msingi,” na, “Jiwe ambalo litawafanya watu wajik wae; mwamba ambao utawafanya waanguke.” Wanajikwaa kwa sababu hawatii lile neno, kama walivyopangiwa tangu mwanzo.

Lakini ninyi ni uzao mteule, ukuhani mtukufu, taifa taka tifu, watu pekee wa Mungu mlioteuliwa kutangaza matendo makuu ya aliyewaita kutoka gizani na kuwaingiza katika nuru yake ya ajabu. 10 Hapo mwanzo ninyi mlikuwa si taifa, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu. Hapo mwanzo mlikuwa hamjapata rehema, lakini sasa mme pata rehema.

11 Rafiki wapendwa, ninawasihi, mkiwa kama wageni na wapi taji njia hapa duniani, epukeni tamaa mbaya za mwili ambazo hupi gana vita na roho zenu. 12 Muwe na mwenendo mwema kati ya watu wasiomjua Mungu, ili kama watawasema kuwa wakosaji, wayaone matendo yenu mema na wamtukuze Mungu siku ile atakapotujia.

Kuwatii Wenye Mamlaka

13 Jinyenyekezeni kwa ajili ya Bwana chini ya mamlaka yote ya wanadamu: ikiwa ni mfalme ambaye ana mamlaka ya mwisho; 14 au ikiwa ni wakuu wengine ambao amewateua kuwaadhibu wahalifu na kuwasifu watendao mema. 15 Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema myazime maneno ya kijinga ya watu wapumbavu. 16 Ishini kama watu huru lakini msitumie uhuru wenu kama kisin gizio cha kutenda uovu; bali muishi kama watumishi wa Mungu. 17 Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu waamini. Mcheni Mungu. Mheshimuni mfalme. 18 Ninyi watumwa, watiini mabwana wenu kwa heshima yote, si wale mabwana walio wapole na wema peke yao, bali hata wale walio wakali. 19 Maana ni jambo jema kwa mtu kuvumilia taabu za maonevu kwa kukumbuka kuwa Mungu yupo. 20 Maana ni sifa gani kwa mtu kustahimili kupigwa kwa kuwa ametenda uovu? Lakini kama mkis tahimili mateso kwa kutenda wema, mnapata kibali mbele za Mungu. 21 Ninyi mmeitwa kwa ajili hiyo, kwa sababu Kristo naye aliteseka kwa ajili yenu akawaachia kielelezo, mzifuate nyayo zake. 22 Yeye hakutenda dhambi wala neno la udanganyifu haliku pita kinywani mwake. 23 Walipomtukana, yeye hakuwarudishia matu kano; alipoteswa, hakuwatishia, bali alimtegemea Mungu ahukumuye kwa haki. 24 Yeye mwenyewe alizibeba juu mtini dhambi zetu mwil ini mwake, ili tuwe wafu kwa mambo ya dhambi na tupate kuishi katika haki. Kwa majeraha yake, ninyi mmeponywa.

25 Kwa maana mlikuwa mmepotea kama kondoo, lakini sasa mmer udi kwa Mchungaji na Mlinzi wa roho zenu.

Therefore, rid yourselves(A) of all malice and all deceit, hypocrisy, envy, and slander(B) of every kind. Like newborn babies, crave pure spiritual milk,(C) so that by it you may grow up(D) in your salvation, now that you have tasted that the Lord is good.(E)

The Living Stone and a Chosen People

As you come to him, the living Stone(F)—rejected by humans but chosen by God(G) and precious to him— you also, like living stones, are being built(H) into a spiritual house[a](I) to be a holy priesthood,(J) offering spiritual sacrifices acceptable to God through Jesus Christ.(K) For in Scripture it says:

“See, I lay a stone in Zion,
    a chosen and precious cornerstone,(L)
and the one who trusts in him
    will never be put to shame.”[b](M)

Now to you who believe, this stone is precious. But to those who do not believe,(N)

“The stone the builders rejected(O)
    has become the cornerstone,”[c](P)

and,

“A stone that causes people to stumble
    and a rock that makes them fall.”[d](Q)

They stumble because they disobey the message—which is also what they were destined for.(R)

But you are a chosen people,(S) a royal priesthood,(T) a holy nation,(U) God’s special possession,(V) that you may declare the praises of him who called you out of darkness into his wonderful light.(W) 10 Once you were not a people, but now you are the people of God;(X) once you had not received mercy, but now you have received mercy.

Living Godly Lives in a Pagan Society

11 Dear friends,(Y) I urge you, as foreigners and exiles,(Z) to abstain from sinful desires,(AA) which wage war against your soul.(AB) 12 Live such good lives among the pagans that, though they accuse you of doing wrong, they may see your good deeds(AC) and glorify God(AD) on the day he visits us.

13 Submit yourselves for the Lord’s sake to every human authority:(AE) whether to the emperor, as the supreme authority, 14 or to governors, who are sent by him to punish those who do wrong(AF) and to commend those who do right.(AG) 15 For it is God’s will(AH) that by doing good you should silence the ignorant talk of foolish people.(AI) 16 Live as free people,(AJ) but do not use your freedom as a cover-up for evil;(AK) live as God’s slaves.(AL) 17 Show proper respect to everyone, love the family of believers,(AM) fear God, honor the emperor.(AN)

18 Slaves, in reverent fear of God submit yourselves to your masters,(AO) not only to those who are good and considerate,(AP) but also to those who are harsh. 19 For it is commendable if someone bears up under the pain of unjust suffering because they are conscious of God.(AQ) 20 But how is it to your credit if you receive a beating for doing wrong and endure it? But if you suffer for doing good and you endure it, this is commendable before God.(AR) 21 To this(AS) you were called,(AT) because Christ suffered for you,(AU) leaving you an example,(AV) that you should follow in his steps.

22 “He committed no sin,(AW)
    and no deceit was found in his mouth.”[e](AX)

23 When they hurled their insults at him,(AY) he did not retaliate; when he suffered, he made no threats.(AZ) Instead, he entrusted himself(BA) to him who judges justly.(BB) 24 “He himself bore our sins”(BC) in his body on the cross,(BD) so that we might die to sins(BE) and live for righteousness; “by his wounds you have been healed.”(BF) 25 For “you were like sheep going astray,”[f](BG) but now you have returned to the Shepherd(BH) and Overseer of your souls.(BI)

Footnotes

  1. 1 Peter 2:5 Or into a temple of the Spirit
  2. 1 Peter 2:6 Isaiah 28:16
  3. 1 Peter 2:7 Psalm 118:22
  4. 1 Peter 2:8 Isaiah 8:14
  5. 1 Peter 2:22 Isaiah 53:9
  6. 1 Peter 2:25 Isaiah 53:4,5,6 (see Septuagint)