16 “Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkapoteza imani yenu. Watawatenga na kuwatoa katika ushirika wa masinagogi. Na si hivyo tu, bali utafika wakati ambapo mtu ye yote atakayewaua atadhani kuwa anamtumikia Mungu. Watu watawatendea haya kwa sababu hawamfahamu Baba wala hawanifahamu mimi. Lakini nimew aambia mambo haya kusudi muda huo utakapofika mkumbuke kuwa nili kuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.

Kazi Ya Roho Mtakatifu

“Lakini sasa ninakwenda kwake yeye aliyenituma, wala hakuna mmoja wenu anayeniuliza, ‘Unakwenda wapi?’ Kwa kuwa nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni. Lakini nawaambia kweli kwamba kuondoka kwangu ni kwa faida yenu kwa maana nisipoondoka, yule Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda nitamtuma aje kwenu. Naye akija atauthibitishia ulim wengu kuhusu dhambi, haki na hukumu. Kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini; 10 kuhusu haki kwa sababu ninakwenda kwa Baba na hamtaniona tena; 11 na kuhusu hukumu kwa sababu mtawala wa ulim wengu huu amekwisha kuhukumiwa.

12 “Nina mambo mengi zaidi ya kuwaambia lakini hamwezi kuy apokea sasa. 13 Akija yule Roho wa kweli atawaongoza muijue kweli yote. Yeye hatanena kwa uwezo wake mwenyewe bali atanena yote atakayosikia. Atawafundisha kuhusu mambo yote yajayo. 14 Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwaambia ninyi. 15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu, ndio maana nimesema kuwa atachukua yaliyo yangu na kuwaambia ninyi.

Huzuni Na Furaha

16 “Baada ya muda mfupi hamtaniona tena; na kisha muda mfupi baadaye mtaniona.” 17 Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Baada ya muda mfupi hamtaniona tena na muda mfupi baadaye mtaniona’? Na ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa baba’?” 18 Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘muda mfupi?’ Hatuelewi ana maana gani!”

19 Yesu alitambua walilotaka kumwuliza kwa hiyo akawaambia, “Mnaulizana nina maana gani nisemapo, ‘Baada ya muda mfupi ham taniona tena na baada ya muda mfupi mtaniona?’ 20 Ninawaambia yaliyo hakika kwamba mtalia na kuomboleza lakini ulimwengu utafu rahi. Mtahuzunika lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha. 21 Mwanamke akaribiapo kuzaa huwa na huzuni kwa sababu saa yake ya uchungu imefika. Lakini mtoto azaliwapo mama anasahau mateso hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto duniani. 22 Na ninyi sasa mna huzuni lakini nitawaona tena na mtafurahi, wala hakuna atakayewaondolea furaha yenu. 23 Wakati huo hamtaniomba kitu cho chote. Ninawaambia kweli kwamba Baba yangu atawapa lo lote mta kaloomba kwa jina langu. 24 Mpaka sasa hamjaomba lo lote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapewa ili furaha yenu ipate kukamil ika.

Ushindi

25 “Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Lakini wakati unakuja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nita waeleza wazi wazi kuhusu Baba yangu. 26 Wakati huo mtaomba kwa jina langu. Wala sisemi kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu; 27 kwa maana Baba mwenyewe anawapenda kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Baba. 28 Nilitoka kwa Baba na nimekuja ulimwenguni, tena sasa naondoka ulimwenguni na ninak wenda kwa Baba.” 29 Wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza wazi wazi wala si kwa mafumbo. 30 Sasa tumejua kwamba wewe una jua mambo yote wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa hiyo tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.” 31 Yesu akawajibu, “Sasa mnaamini? 32 Saa inakuja, tena imeshawadia, ambapo mtata wanyika, kila mtu aende nyumbani kwake na kuniacha peke yangu; lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yuko pamoja nami. 33 Nimewaambia mambo haya ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”

16 “All this(A) I have told you so that you will not fall away.(B) They will put you out of the synagogue;(C) in fact, the time is coming when anyone who kills you will think they are offering a service to God.(D) They will do such things because they have not known the Father or me.(E) I have told you this, so that when their time comes you will remember(F) that I warned you about them. I did not tell you this from the beginning because I was with you,(G) but now I am going to him who sent me.(H) None of you asks me, ‘Where are you going?’(I) Rather, you are filled with grief(J) because I have said these things. But very truly I tell you, it is for your good that I am going away. Unless I go away, the Advocate(K) will not come to you; but if I go, I will send him to you.(L) When he comes, he will prove the world to be in the wrong about sin and righteousness and judgment: about sin,(M) because people do not believe in me; 10 about righteousness,(N) because I am going to the Father,(O) where you can see me no longer; 11 and about judgment, because the prince of this world(P) now stands condemned.

12 “I have much more to say to you, more than you can now bear.(Q) 13 But when he, the Spirit of truth,(R) comes, he will guide you into all the truth.(S) He will not speak on his own; he will speak only what he hears, and he will tell you what is yet to come. 14 He will glorify me because it is from me that he will receive what he will make known to you. 15 All that belongs to the Father is mine.(T) That is why I said the Spirit will receive from me what he will make known to you.”

The Disciples’ Grief Will Turn to Joy

16 Jesus went on to say, “In a little while(U) you will see me no more, and then after a little while you will see me.”(V)

17 At this, some of his disciples said to one another, “What does he mean by saying, ‘In a little while you will see me no more, and then after a little while you will see me,’(W) and ‘Because I am going to the Father’?”(X) 18 They kept asking, “What does he mean by ‘a little while’? We don’t understand what he is saying.”

19 Jesus saw that they wanted to ask him about this, so he said to them, “Are you asking one another what I meant when I said, ‘In a little while you will see me no more, and then after a little while you will see me’? 20 Very truly I tell you, you will weep and mourn(Y) while the world rejoices. You will grieve, but your grief will turn to joy.(Z) 21 A woman giving birth to a child has pain(AA) because her time has come; but when her baby is born she forgets the anguish because of her joy that a child is born into the world. 22 So with you: Now is your time of grief,(AB) but I will see you again(AC) and you will rejoice, and no one will take away your joy.(AD) 23 In that day(AE) you will no longer ask me anything. Very truly I tell you, my Father will give you whatever you ask in my name.(AF) 24 Until now you have not asked for anything in my name. Ask and you will receive,(AG) and your joy will be complete.(AH)

25 “Though I have been speaking figuratively,(AI) a time is coming(AJ) when I will no longer use this kind of language but will tell you plainly about my Father. 26 In that day you will ask in my name.(AK) I am not saying that I will ask the Father on your behalf. 27 No, the Father himself loves you because you have loved me(AL) and have believed that I came from God.(AM) 28 I came from the Father and entered the world; now I am leaving the world and going back to the Father.”(AN)

29 Then Jesus’ disciples said, “Now you are speaking clearly and without figures of speech.(AO) 30 Now we can see that you know all things and that you do not even need to have anyone ask you questions. This makes us believe(AP) that you came from God.”(AQ)

31 “Do you now believe?” Jesus replied. 32 “A time is coming(AR) and in fact has come when you will be scattered,(AS) each to your own home. You will leave me all alone.(AT) Yet I am not alone, for my Father is with me.(AU)

33 “I have told you these things, so that in me you may have peace.(AV) In this world you will have trouble.(AW) But take heart! I have overcome(AX) the world.”