Salamu Kwa Watu Mbalimbali

16 Napenda kumtambulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika Kanisa la Kenkrea. Mpokeeni kama dada yenu katika Kristo, jinsi iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wow ote atakaohitaji kutoka kwenu maana yeye amekuwa msaada kwa watu wengi, pamoja na mimi.

Salamu zangu kwa Priska na Akila, watumishi wenzangu katika huduma ya Kristo Yesu. Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Mimi ninawashukuru wao; na si mimi tu bali pia makanisa yote ya watu wa mataifa mengine. Natoa salamu pia kwa lile kanisa linaloabudu nyumbani kwao. Msalimuni rafiki yangu Epaineto aliyekuwa mtu wa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo.

Salamu zangu kwa Maria aliyefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu. Wasalimuni Andronika na Yunia, jamaa zangu ambao wamekuwa gerezani pamoja nami. Wao ni maarufu miongoni mwa mitume, na walimfahamu Kristo kabla yangu. Salamu zangu kwa Ampliato, mpendwa wangu katika Bwana. Salamu zangu kwa Urbano mfanyakazi mwenzetu katika utumishi wa Kristo pamoja na rafiki yangu mpendwa Stakisi. 10 Salamu zangu kwa Apele ambaye amethibitisha imani yake kwa Kristo. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani kwa Aristobulo. 11 Salamu zangu kwa ndugu yangu Herodioni, na kwa wote walio nyumbani kwa Narkisi wanaomwamini Bwana. 12 Salamu zangu kwa Trifainia na Trifosa, wakina mama wanaofanya kazi kwa bidii katika Bwana. Msalimuni mpendwa wangu Persisi ambaye pia ni mama mwingine aliyemtumikia Bwana kwa bidii. 13 Salamu zangu kwa Rufo, mteule wa Bwana na mama yake, ambaye amekuwa kama mama yangu pia. 14 Wasalimuni Asinkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao. 15 Salamu zangu kwa Filologona na Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa na watu wote wa Mungu walio pamoja nao. 16 Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu. Ndugu wa makanisa yote ya

Maonyo Ya Mwisho

17 Ndugu zangu, nawasihi mjihadhari na wote wanaoleta mafara kano na vipingamizi kinyume cha mliyopokea. Waepukeni. 18 Kwa maana watu kama hao hawamtumikii Bwana Kristo, bali wanatumikia tamaa zao wenyewe. Kwa kutumia maneno matamu ya kudanganya, hupo tosha mioyo ya watu wanyofu. 19 Kila mtu amesikia juu ya utii wenu na nimekuwa na furaha kwa ajili yenu. Lakini napenda muwe na hekima katika mambo mema na bila hatia katika mambo maovu. 20 Na Mungu wa amani hatakawia kumponda shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu iwe pamoja nanyi. 21 Timotheo, mfanyakazi mwenzangu anawasalimu. Mnasalimiwa pia na Lukio, Yasoni, na Sosipatro, ndugu zangu. 22 Na mimi Tertio niliyem wandishi wa barua hii nawasalimia kama ndugu yenu katika Kristo. 23 Salamu kutoka kwa Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote la hapa. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto pia wanawasalimu. [ 24 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe pamoja nanyi nyote. Amina].

Sala Ya Kumsifu Mungu

25 Na asifiwe Mungu ambaye anaweza kuwaimarisha katika Injili niliyowahubiria juu ya Yesu Kristo, kulingana na mafunuo ambayo yalikuwa yamefichika tangu zamani za kale; 26 lakini ambayo sasa yamewekwa wazi na kwa njia ya Maandiko ya manabii yamedhihirishwa kwa mataifa yote kwa amri ya Mungu wa milele, wapate kumwamini na kumtii. 27 Mungu aliye pekee mwenye hekima, atukuzwe milele na milele kwa njia ya Yesu Kristo! Amina.

Personal Greetings

16 I commend(A) to you our sister Phoebe, a deacon[a][b] of the church in Cenchreae.(B) I ask you to receive her in the Lord(C) in a way worthy of his people(D) and to give her any help she may need from you, for she has been the benefactor of many people, including me.

Greet Priscilla[c] and Aquila,(E) my co-workers(F) in Christ Jesus.(G) They risked their lives for me. Not only I but all the churches of the Gentiles are grateful to them.

Greet also the church that meets at their house.(H)

Greet my dear friend Epenetus, who was the first convert(I) to Christ in the province of Asia.(J)

Greet Mary, who worked very hard for you.

Greet Andronicus and Junia, my fellow Jews(K) who have been in prison with me.(L) They are outstanding among[d] the apostles, and they were in Christ(M) before I was.

Greet Ampliatus, my dear friend in the Lord.

Greet Urbanus, our co-worker in Christ,(N) and my dear friend Stachys.

10 Greet Apelles, whose fidelity to Christ has stood the test.(O)

Greet those who belong to the household(P) of Aristobulus.

11 Greet Herodion, my fellow Jew.(Q)

Greet those in the household(R) of Narcissus who are in the Lord.

12 Greet Tryphena and Tryphosa, those women who work hard in the Lord.

Greet my dear friend Persis, another woman who has worked very hard in the Lord.

13 Greet Rufus,(S) chosen(T) in the Lord, and his mother, who has been a mother to me, too.

14 Greet Asyncritus, Phlegon, Hermes, Patrobas, Hermas and the other brothers and sisters with them.

15 Greet Philologus, Julia, Nereus and his sister, and Olympas and all the Lord’s people(U) who are with them.(V)

16 Greet one another with a holy kiss.(W)

All the churches of Christ send greetings.

17 I urge you, brothers and sisters, to watch out for those who cause divisions and put obstacles in your way that are contrary to the teaching you have learned.(X) Keep away from them.(Y) 18 For such people are not serving our Lord Christ,(Z) but their own appetites.(AA) By smooth talk and flattery they deceive(AB) the minds of naive people. 19 Everyone has heard(AC) about your obedience, so I rejoice because of you; but I want you to be wise about what is good, and innocent about what is evil.(AD)

20 The God of peace(AE) will soon crush(AF) Satan(AG) under your feet.

The grace of our Lord Jesus be with you.(AH)

21 Timothy,(AI) my co-worker, sends his greetings to you, as do Lucius,(AJ) Jason(AK) and Sosipater, my fellow Jews.(AL)

22 I, Tertius, who wrote down this letter, greet you in the Lord.

23 Gaius,(AM) whose hospitality I and the whole church here enjoy, sends you his greetings.

Erastus,(AN) who is the city’s director of public works, and our brother Quartus send you their greetings. [24] [e]

25 Now to him who is able(AO) to establish you in accordance with my gospel,(AP) the message I proclaim about Jesus Christ, in keeping with the revelation of the mystery(AQ) hidden for long ages past, 26 but now revealed and made known through the prophetic writings(AR) by the command of the eternal God, so that all the Gentiles might come to the obedience that comes from[f] faith(AS) 27 to the only wise God be glory forever through Jesus Christ! Amen.(AT)

Footnotes

  1. Romans 16:1 Or servant
  2. Romans 16:1 The word deacon refers here to a Christian designated to serve with the overseers/elders of the church in a variety of ways; similarly in Phil. 1:1 and 1 Tim. 3:8,12.
  3. Romans 16:3 Greek Prisca, a variant of Priscilla
  4. Romans 16:7 Or are esteemed by
  5. Romans 16:24 Some manuscripts include here May the grace of our Lord Jesus Christ be with all of you. Amen.
  6. Romans 16:26 Or that is